Kupakua fomu hili, bonyeza: VITUO ATAMIZI VYA KILIMOBOASHARA VYA AIC
VITUO ATAMIZI VYA KILIMOBIASHARA VYA AIC,
TANGAZO KWA VIJANA
FURSA YA KUJIUNGA 2021/22
Kituo cha Ubunifu wa Kilimobiashara (AIC), ambacho ni idara ya Taasisi ya PASS inapenda kuwatangazia vijana wenye nia ya kufanya kilimobiashara kwamba inapokea maombi ya kujiunga na Vituo Atamizi vya Kilimobiashara vilivyopo SUA Morogoro na TALIRI Farm, Mbande, Kongwa mkoani Dodoma.
Katika vituo hivi, AIC inawapa fursa vijana ya kuanzisha, kumiliki na kuendesha kilimobiashara kwenye sekta ndogo ya mboga na matunda, mifugo na nyama.
Kijana atakayeomba nafasi hii anatakiwa awe na uzoefu wa mwaka mmoja kwenye kilimo biashara, tabia njema, mtiifu, mwenye nidhamu, mchapakazi, fikra chanya, mwaminifu na anayependa kuona matokeo chanya. Vijana wa Kike watapewa Kipaumbele.
Vijana washiriki kwenye Vituo Atamizi watakopeshwa vifaa, miundo mbinu, na mtaji wa kufanya kilimobiashara ambapo watausimamia kwa kipindi cha miezi 12.
Katika kipindi chote, waatamiwa watapewa usimamizi wa karibu ikiwemo ushauri wa kibiashara na upelembaji, ili kuhakikisha wanafanikiwa katika shughuli zao za kilimobiashara. Kila mshiriki anatakiwa athibitishe kuwa na eneo linalofaa kwa kilimo biashara kabla ya kujiunga na kituo atamizi ili baada ya kuhitimu, vijana watakaofanikiwa, waweze kuanzisha biashara kama hiyo kwenye maeneo yao.
Vijana wenye nia wanashauriwa kutuma maombi yao ya kujiunga na kituo Atamizi kimojawapo kati ya SUA-AIC Morogoro kinachojihusisha na kilimobiashara cha mboga na matunda au AIC Kongwa kilichopo Taliri Farm (PRC), Mbande kinachojihusisha na biashara ya unenepeshaji/ufugaji mbuzi na usindikaji wa nyama ya mbuzi. Vijana 250 watachaguliwa kwenye awamu ya kwanza ya mchujo na kati ya hawa, vijana 100 (80 Morogoro and 20 Kongwa) watachaguliwa kwenye awamu ya pili ya mchujo kujiunga na Vituo Atamizi kuanzia Oktoba 2021.
Kwa maelezo zaidi na jinsi ya kupata, kujaza na kurudisha fomu ya maombi yanapatikana kwenye tovuti ya www.aic.co.tz na www.pass.or.tz, SUA-SAEBS, ofisi za AIC (SUA, Morogoro na Mbande, Kongwa) na ofisi zote za PASS nchini. Mwisho wa kupokea maombi ni tarehe 15/07/2021 saa 11.00 jioni.